Pemba School of Health Sciences inapenda kuwapongeza wachezaji wa Timu ya Mpira wa Miguu ya PSHS kwa ushindi wao wa kishindo katika mashindano ya michezo ya vyuo vya afya.
Timu yetu imeonesha nidhamu, mshikamano, na juhudi kubwa ambazo zimezaa matunda ya ushindi. Kupitia ushindi huu, timu imepokea zawadi maalum kama ishara ya kuthamini mchango wao katika kuleta heshima kwa taasisi yetu.
Tukio la kukabidhi zawadi lilihudhuriwa na uongozi wa shule, walimu, wanafunzi, pamoja na wageni waalikwa.